Abdulswamad aahidi kuangazia maslahi ya wafanyikazi wa kaunti ya Mombasa
Gavana mteule wa kaunti ya Mombasa Abdulswamad Shariff Nassir ameahidi kuangazia kikamilifu maslahi ya wafanyikazi wa kaunti ya Mombasa ili kuwawezesha kutekeleza majumu yao ipasavyo.
Akiongea katika taasisi ya Mafunzo ya Serikali mjini Mombasa wakati wa kongamano lililowaleta pamoja wenyeviti 47 kutoka bodi za huduma ya Umma kwenye kaunti zote nchini ,Nassir aidha amesema kuwa serikali yake haitawatenga wafanyikazi waliyoandikwa na utawala uliopita kuhudumu kwenye kaunti ya Mombasa.
Wakati huo huo Nassir amesema kuwa kamwe utawala wake hautawachukulia hatua wafanyikazi wa kaunti hiyo waliokuwa na msimamo tofauti wa kisiasa wakati wa kinyang’anyiro cha kuwania kiti cha ugavana kwenye kaunti hiyo, na badala yake amesema kuwa atahakikisha maslahi ya wafanyikazi yanatimizwa.
Aidha wakati wa kongamano hilo Nassir amezirai bodi za huduma ya umma kwenye kaunti zote nchini kuonyesha ushirikiano kwa magavana wapya walioingia madarakani ili kuhakikisha kuwa oparesheni kwenye kaunt zinaendelezwa bila tashwishi.
Haya yanajiri huku maandalizi ya kuapishwa kwa Nassir kuwa gavana mpya wa kaunti ya Mombasa mnamo siku ya Alhamisi yakiendelea katika bustani ya Mama Ngina Water Front.