Wanandondi 13 waondoka kuelekea Cameroon katika michuano ya kufuzu kwa Olimpiki

download (14)

Wanandondi 13 wameelekea jijini Yaunde nchini Cameroon hii leo kushiriki michuano ya kufuzu katika mashindano ya Olimpiki kuanzia tarehe 9 hadi 20.

Patrick Maina na msaidizi wake David Manuhe ni wakufunzi wa timu ya wanandoni  ya wanaume 10 na wanawake 3 wanao tarajiwa kufika Cameroon hii leo.

Meneja wa timu hiyo Stanley Njoroge pamoja na nahodha Nick Abaka kutoka timu ya KDF pia atashiriki mchuano huo .

Afrika wamepewa nafasi 33 za wanaume katika kila kitengo huku kina dada 3 katika uzani wa Flyweight,Lightweight na Middleweight katika michuano hiyo.