Msafara wa Redio Salaam Mombasa(KWA PICHA)
Mamia ya mashabiki wa Idhaa ya radio Salaam wamejitokeza katika barabara za mji wa Mombasa kukutana na watangazaji mahiri wa Idhaa hii.
Wenyeji wa kaunti ya Mombasa wamepata fursa ya kutangamana na watangazaji wa idhaa ya radio salaam pamoja na kujishindia zawadi kem kem.
Msafara huo umepitia barabara mbali mbali za mji wa Mombasa huku kilele kikiwa mjumuiko mkubwa katika uwanja wa Mama Ngina.
Meneja wa mauzo wa Radio Salaam Alice Odindi amewashukuru mashabiki kwa kujitokeza kwa wingi akisema ni fursa kwa wao kushinda zawadi kem kem huku akiwashukuru wasikilizaji wa idhaa hii kwa kuendelea kuinga mkono.
Hapo kesho, msafara huo utaelekea maeneo ya Mtwapa, Kilifi na kilele kikiwa katika uwanja wa Karisa Maitha mjini Malindi mwendo wa saa kumi jioni.