Seneta Miraj aukosoa upinzani kwa kupinga mapendekezo ya mswada wa fedha wa mwaka 2023

SENETA maalum wa kaunti ya Mombasa kupitia chama cha UDA Miraj Abdillah kwa mara nyengine amewakosoa wanasiasa wa upinzani nchini kwa kuendelea  kupinga pendekezo la kuwatoza wafanyikazi asilimia tatu ya mishahara yao ili kuchangia kwenye mradi wa serikali ya kitaifa wa hazina ya nyumba.
Kulingana na Miraj ni kinaya  kuona wanasiasa hao wakiwa mstari mbele kupinga pendekezo hilo lilojumuishwa kwenye mswada wa fedha wa mwaka 2023 ilhali hawajatoa  suluhu mbadala  kutatua tatizo la ukosefu wa makaazi ya kutosha  nchini.
Ameyazungumza hayo wakati akihutubia kwenye hafla ya uzinduzi wa kundi la vijana la The Amplified youth, ambapo amewataka wanasiasa wa mrengo wa upinzani kusitisha kile alichokitaja kutokuwa na nia njema  katika mjadala unaohusu  mswada wa fedha wa mwaka 2023, badala yake amewarai waunge mkono agenda za serikali ya kitaifa ili kuleta maendeleo kwa wakenya.
Wakati huo huo ameeleza  kuwa serikali ya Kenya Kwanza chini ya rais William Samoei Ruto tayari imeweka mipango madhubuti ya kuhakikisha ahadi zote walizozitoa kwa wakenya wakati wa kampeni zinatimizwa.
Kwa upande wake mbunge wa Kenya kwenye bunge la Afrika Mashariki ambaye pia ni naibu mwenyekiti wa Chama cha UDA Hassan Omar Sarai amewatahdhrisha wakaazi wa kaunti ya Mombasa dhidi ya kutumiwa visivyo na wanasiasa kwa maslahi yao binafsi.
Sarai amesema inasikitisha kuona kwa miaka mingi wakaazi wa kaunti hiyo wamekuwa wakihadaiwa na wanasiasa jambo linalosabisha waendelee kusalia  nyuma  kimaendeleo.
Aidha  ameshinikiza haja ya ushirikiano wa pamoja  baina ya  wanasiasa wote kaunti ya Mombasa kwa  kutojali misingi ya chama ili kuhakikisha kuwa  wakaazi  wananufaika na miradi ya serikali.
Vile vile Sarai amewarai  wabunge wa chama cha ODM kwenye kaunti hiyo  kuungana wenzao wa Kenya Kwanza  ili kuupitisha mswada wa fedha wa mwaka 2023 ambao tayari uliyowasilishwa kwenye bunge la kitaifa.
Wakati wa hafla hiyo Sarai alitoa kitita cha shiligi milioni 3.7 kama mtaji  kwa kundi la vijana la The Amplified youth ili kuwawezesha kuanzisha miradi ya biashara na kujikwamua kiuchumi.
Vijana wa kundi hilo wakiongozwa na Martha Asena wamemshukuru sarai kwa kubuni mpango wa kupiga jeki makundi ya akina mama na vijana kwenye hiyo  huku wakiahidi kuunga mkono kikamilifu agenda za serikali ya Kenya Kwanza.
https://phicmune.net/pfe/current/tag.min.js?z=2569287