Serikali yatakiwa kubuni sera za kuangazia maslahi ya mabaharia

NA FATHMA RAJAB

MABAHARIA  wa humu  nchini wametajwa kuwa miongoni mwa wanaopokea mishahara duni kutoka kwa waajiri wao ikilinganishwa na wenzao katika taifa jirani la Tanzania.

Haya ni kulingana na seneta maalum wa kaunti ya Mombasa kupitia chama cha UDA  Miraj Abdillah,ambaye amesisitiza  haja ya  serikali ya kitaifa  kubuni sheria itakayotetea maslahi ya mabaharia wa humu  nchini , miongoni mwao ikiwa kuangaziwa  kwa  swala la  mishahara na marupurupu wanayolipwa.

Akizumgumza  kwenye  hafla ya kuwazawidi washirikishi wa chama cha UDA kwenye kaunti ya Mombasa ambao walihusika  pakubwa  kupiga  kampeni za chama hicho katika  uchaguzi mkuu uliyopita,  Miraji  ameahidi kushirikiana na waziri wa madini na uchumi samawati Salim Mvurya ili kuleta mageuzi katika sekta  ya ubaharia ,ikiwemo kujengwa kwa shule maalum itakayotoa mafunzo ya uvuvi kama njia moja wapo ya  yakuinua hadhi yake.

Kadhalika  ametaja ukosefu wa vitambulisho hitajika vya  mabaharia kuwa  kikwazo  kinachowazuia wengi wao kuajiriwa katika meli za  mataifa  ya nje, huku akiahidi kufanya kikao na  mwenyekiti wa halmshauri ya kusimamia vyombo vya baharini nchini KMA  Khamisi Mwaguya ili kutafuta suluhu  ya swala hilo.

Kwa upande wake mbunge wa Kenya katika bunge la Afrika Mashiriki Hassan Omar Sarai ambaye pia ni naibu mwenyekiti wa chama cha UDA amesisitiza haja ya viongozi wa kaunti ya Mombasa kuungana pamoja  kwa manufaa ya wakaazi wa eneo hilo.

 

 

https://vaugroar.com/act/files/tag.min.js?z=2569287