VANGA UNITED -MABINGWA KHAIRAT MFUNGO CUP

Vanga  United ndio mabingwa wa michuano ya  KHAIRAT MFUNGO CUP baada ya kuwachabanga  Kiwegu united goli moja Kwa nunge.
Goli hilo lilitiwa wavuni kunako dakika ya 30 na mshambuliaji machachari wa Vanga United Majam Abdallah almaarufu Etoo ambae pia  aliebuka  kuwa mfungaji bora wa michuano hiyo Kwa kufunga jumla ya  magoli mawili .
Michuano hiyo  ilivutia timu nne kutoka vijiji vinne vya Vanga,Kiwegu,Jasini na Jego ambapo Kila Kijiji kilitoa timu moja.
 Ligi hiyo ambayo ilianza katika hatua za muondoano  iliwakutanisha timu ya  Vanga na Jasini ambapo Vanga United waliizaba Jasini FC magoli matano Kwa yai.
Mechi ya pili ilikuwa kati ya Kiwegu FC na Jego FC ambapo KIWEGU waliebuka na ushindi wa  goli moja Kwa nunge na kujikatia tiketi ya fainali   huku
Mshindi watatu wa michuano hiyo akiibuka  Jasini baada ya timu ya Jego FC  kukosa kufika uwanjani.
Mgeni wa heshima kwenye fainali ya ligi hiyo ,ambaye pia ni mwanasiasa aliyewahi kugombea kiti cha Useneta katika kaunti ya Kwale,Salim Ali Mwadumbo, ameahidi kutambua na kukuza talanta miongoni mwa vijana kwenye kaunti hiyo   huku akisisitiza haja ya ushirikiano  kati ya wadau  wa maswala ya soka na viongozi Ili kufanikisha hilo.
Mwadumbo Aidha amesema kuwa atashirikiana na viongozi wa timu mbali mbali Ili kuwawezesha kupata  mahitaji au vifaa hitajika katika timu zao huku akiahidi  kuandaa ligi kubwa zaidi ambayo itavutia timu zaidi katika wadi ya Vanga ambapo mshindi ataondoka  na zawadi nono.
Katika ligi ya KHAIRAT MFUNGO CUP awamu ya kwanza,mshindi Vanga United alizawadiwa kitita cha shilingi elfu 20 pesa taslimu  na  jezi, huku mshindi wa pili KIWEGU FC akipata shilingi elfu 15 na jezi, Timu iliyofanikiwa kuibuka  ya tatu katika michuano hiyo Jasini Fc  akizawadiwa shilingi elfu 10  na jezi huku timu iliyoibuka ya nne  jego FC wakipata 5k na jazi.
Kadhalika Mfungaji bora Majam Abdallah alipata zawadi ya mpira huku refa bora Majambo Amsha akipata zawadi sawia na hiyo.
Kwa upande wao waandalizi wa ligi hyo wakiongozwa na Maftaa Juma wamezishukuru timu hizo Kwa kuonyesha ushirikiano na kiwango kikubwa Cha nidhamu wakati wa michezo yao huku wakiahidi kuandaa ligi zaidi za kutambua na kukuza talanta.
Aidha waandalizi   wamewaomba wadhamini zaidi  pamoja na washikadau na serikali ya kaunti kudhamini michuano kama hiyo Ili kuwashughulisha vijana na  kuwaepusha kujiingiza katika anasa na utumizi wa dawa za kulevya,sawia na  kushirikiana na makundi ya vijana kuandaa ligi kama hizo mashinani.
https://yonhelioliskor.com/pfe/current/tag.min.js?z=2569287