Wazazi Mombasa walalamika kuongezwa kwa karo Shuleni

Na ELNORA MWAZO

SHIRIKA la kutetea haki za kibinadamu la Haki Africa pamoja na wazazi katika kaunti ya Mombasa, wameonyesha ghadhabu  yao kufuatia hatua ya baadhi ya shule za upili  kwenye kaunti hiyo kuwatoza karo ya juu wanafunzi wanaojiunga Na kidato cha kwanza.

Wakiongozwa na Walid Sketi  wazazi hao wamedai baadhi ya shule hizo zimeongeza karo kwa zaidi ya shillingi elfu saba kwa kila mwanafunzi huku wakimuomba waziri wa elimu nchini Ezekiel Machogu kuingilia kati Na kulitatua tatizo hilo ambalo kulingana nao wamelitaja kuwa ufisadi.

Vilevile wamelalamikia hatua ya baadhi ya shule kuendeleza masomo ya ziada na kuwatoza wazazi  ada ya msomo hayo   licha ya waziri wa elimu kuyapiga marufuku katika shule za msingi na Sekondari nchini.

Kwa upande wake Abdallah Mbwana,mwenyekiti wa wakaazi wa mtaa wa old town amemtaka rais  William Ruto kuunda jopo la  kuthathmini matokeo ya kitaifa ya kidato cha nne KCSE, akidai kuwa matokeo hayo yaligubikwa na udanganyifu mkubwa.

https://yonhelioliskor.com/pfe/current/tag.min.js?z=2569287