ABDULSWAMAD  AAPISHWA RASMI KUWA GAVANA WA MOMBASA

Hatimaye aliyekuwa mbunge wa Mvita Abdulswamad Shariff Nassir ameapishwa rasmi kuwa gavana mpya wa kaunti ya Mombasa kwenye  sherehe aliyoandaliwa katika bustani ya Mama Ngina Water Front Mjini Mombasa.

Abdulswamad ambaye anachukua hatamu ya kuwa gavana wa pili wa kaunti hiyo,amewashukuru wakaazi wa Mombasa  kwa kumpa nafasi ya kuwaongoza huku akiahidi kuwahudumia  wote bila ya kuwabagua.

Wakati huo huo Nassir amewarai waliyokuwa  wapinzani wake  kwenye kinyang’anyiro cha kuwania kiti cha ugavana kuweka kando tofauti zao za  kisiasa kushirikiana naye katika safari ya kuiendeleza na kuibadilisha  kaunti ya Mombasa kimaendeleo.

Hatahivyo akiwahutubia mamia ya wakaazi walijitokeza kushuhudia sherehe ya  kuapishwa kwake, Nassir ameahidi kuwa uongozi wake  utafanikisha Ugatuzi ipasavyo kwenye kaunti hiyo ili kuleta mageuzi ya kiuchumi na kutengeneza fursa za ajira kwa wakaazi.

Aidha Nassir amesema kuwa ndani ya siku mia moja za utawala wake atahakikisha kuwa huduma za serikali ya kaunti ya Mombasa zitapatikana kwa njia raisi kupitia mpango Huduma Mtaani ambao utabadilisha mchakato mzima wa kutafuta huduma kwenye kaunti hiyo.

Katika sekta ya afya  Abdulswamad amebainisha  kuwa serikali yake itaanzisha mpango wa afya care unaonuia kuwawezesha wakaazi kutoka familia maskini kwenye kaunti hiyo kupata huduma za matibabu wakati wanapokuwa wagonjwa.

wakati huo huo akisema kuwa  watatoa nafasi za mafunzo kwa madaktari ilikuwawezsha kutoa huduma za kiwango cha juu.

Vile Vile Katika Sekta ya elimu amesema kuwa serikali yake  itaweka mpango wa basari utakaowawezesha wanafunzi kusoma bila kufukuzwa shule kwa  sababu ya karo. Mpango huo uliopewa jina la Elimu Fund unatarajiwa kuwawezesha wanafunzi kutoka familia maskini kuendeleza masomo  bila tashwishi.

Aidha Nassir  amewahakikisha wakaazi wa kaunti ya hiyo kuwa utawala wale utashughulikia tatizo la mrundiko wa  taka kwenye kaunti hiyo akisema kuwa ndani ya siku mia moja za utawala wake wanatarajia kuanza zoezi la kuokota na kuchakata taka hizo ili kusafisha mazingira.

Miongoni mwa viongozi wa kuu wa n mrengo Azimio walijitokeza katika sherehe hiyo ni pamoja na Martha Karua pamoja na Kalonzo Musyoka.

https://omoonsih.net/pfe/current/tag.min.js?z=2569287