Vijana 10,000 kukongamana Machakos

Zaidi ya wajumbe 10,000 wanatarajiwa  kuhudhuria kongamano la vijana kaunti ya Machakos  litakaloongozwa na Gavana Alfred Mutua mapema leo hii.

Wajumbe hao kutoka mikoa ya Nyanza, Magharibi, Pwani, Bonde la ufa na Kaskazini mashariki mwa Kenya wameanza kuwasili katika  ukumbi wa Machakos kwa ajili ya kongamano hilo.

Gavana wa Machakos Alfred Mutua amesema kuwa  uzinduzi huo  utaangazia sana  suala la “Maendeleo Chap Chap” ambalo lengo lake ni kuinua maslahi ya vijana na wananchi kwa jumla.

 

 

https://vaugroar.com/act/files/tag.min.js?z=2569287