Raia wa Jordan waliyokamatwa Mombasa wakiomba waregeshwa kwao

Raia arubaini wa Jordan waliokamatwa na maafisa wa polisi wiki moja iliyopita mjini Mombasa wakiomba  katika mtaa wa Old Town wameregeshwa nchini mwao.

Watalii hao ambao walikamatwa kwa kosa la kukiuka sheria katika  stakadhi zao za visa  wanajumuisha watu wazima 19 pamoja na watoto 21, mdogo wao zaidi akiwa na umri wa miezi minne.

Hatahivyo akiongea na wanahabari  mjini Mombasa wakati  akisisimamia safari ya watalii hao Mwakilishi wadi wa eneo  la Tudor Samir Balo amedokeza kuwa msaada wa usafiri waliyoupata raia hao wa Jordan Umetoka kwa mfanyibiasha tajika  mjini Mombasa Hasu Patel ambaye aliingilia kati  baada ya kusikia masaibu waliyokuwa wakipitia raia hao wa kigeni.

Awali maafisa kutoka idara ya uhamiaji na makachero kutoka kitengo cha kukabiliana na ulanguzi wa binadamu walikuwa wamewahoji  raia hao wa kigeni lakini bado kufikia sasa hawajatoa ripoti kamili kuhusu uchunguzi wao.

Raia hao wanatarajiwa kusafari hadi Nairobi na kisha kuabiri ndege hadi nchini Jordan hapo kesho.

https://uwoaptee.com/pfe/current/tag.min.js?z=2569287